Gavana wa Machakos Alfred Mutua siku ya Alhamisi alifunga sehemu ya nyama ya Naivas Supermarket katika kaunti yake.
Alifafanua kwamba hatua hiyo ilikuwa inahitajika kufuatia maelezo juu ya kemikali iliyowekwa ndani ya nyama.
Mwanahabari wa NTV, Dennis Okari alifichua siri hiyo ambayo soko ya nyama imekuwa ikitumia kulinda nyama kwa kutoharibika mapema.
Kemikali hizo ambazo zinawekwa kwa nyama kwa mujibu wa daktari, ni hatari kwa mwili na unaweza kusababisha saratani.
CLOSURE OF NAIVAS SUPERMARKETS’ BUTCHERY (MEAT) SECTION IN MACHAKOS COUNTY ON PUBLIC INTEREST
Following a media report on meat that may be unfit for human consumption due to presence of chemicals being sold in supermarkets,….
— Dr. Alfred Mutua (@DrAlfredMutua) July 18, 2019
Gavana Mutua alisema kuwa baada ya kufichuliwa kwa siri hiyo, alichukua hatua ya kupima baadhi ya nyama zinazouzwa kwenye kaunti yake.
“Nimepewa ripoti ya maabara inayoonyesha kwamba sampuli ya nyama iliyouzwa kwenye Naivas Supermarket katika Gateway Mall katika Mavoko, kaunti ya Machakos, ilikuwa na miligramu 3,286 za ziada ambayo haipaswi kutumiwa kwa nyama,” inasoma ujumbe wa gavana.
Bw. Mutua aliongeza kuwa sehemu hizo za nyama zitasalia kufungwa hadi ukaguzi unapofanywa.
I direct my officers in collaboration with National Govt. officers to move with speed to all supermarkets in Machakos County for investigations and advisory to the public.
The butchery sections will remain closed until given an okay to open by my Government’s public health Dept.— Dr. Alfred Mutua (@DrAlfredMutua) July 18, 2019