Yanga Yaicharaza Azam Mkwakwani, Feisali Ashika Kichwa

Mechi ya Ngao ya Hisani iliyokuwa kati ya Yanga na Azam FC imefanyika katika Uwanja wa Mkwakwani. Yanga imefanikiwa kushinda mechi hiyo na hivyo kufuzu kwa fainali itakayosakatwa Jumapili, huku wakisubiri mshindi wa mechi ya kesho kati ya Simba na Singida Fountain Gate pia itakayopigwa katika Uwanja wa Mkwakwani.

Yanga ilifanikiwa kufunga bao lao la kwanza katika dakika za mwisho za mchezo, bao lililofungwa na Aziz K. Bao la pili la Yanga lilifungwa na Mzize, ambaye wote walikuwa wameingia uwanjani kama wachezaji wa akiba kwa kipindi cha pili.

Ushindi huu wa Yanga unawapa tiketi ya kutinga fainali, ambapo watapambana na mshindi wa mechi ya kesho kati ya Simba na Singida Fountain Gate. Mashabiki wa soka nchini Tanzania wanatarajia mechi hiyo ya fainali itakuwa ni mtanange mzuri na wa kusisimua.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *