Maafisa wa polisi hatimaye wamkamata mkurugenzi wa Keroche Tabitha Karanja

Image result for tabitha karanja

Mkurugenzi Mtendaji wa Keroche, Tabitha Karanja mwishowe amekamatwa katika oparesheni kali iliyoongozwa na maafisa wa DCI walioshikamana na maafisa wa Flying Squad.

Karanja alikuwa amezungukwa katika ofisi zake katika makao makuu ya Viwanda vya Keroche huko Naivasha akisema kwamba hatajisalimisha kwa maafisa wa polisi waliotumwa kumkamata.

DPP Noordin Haji Alhamisi jioni aliagiza kukamatwa kwake pamoja na mumewe Joseph Karanja juu ya tuhuma za kukwepa ushuru wa Shilingi 14 bilioni.

Image result for tabitha karanja

Baada ya kuzungukwa kwa masaa 18, Karanja mwishowe alikamatwa na ripoti inasema kuwa maafisa wa DCI walipata kibali cha kumkata Alhamisi asubuhi.

Maelezo zaidi kufuatia…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *