Mpenzi wa zamani wa Diamond Platinumz, Zari Hassan amefichua siri kinachomfanya kuongeza unene hivi karibuni.
Zari ameeleza kuwa anapata dozi nzuri ya ngono kutoka kwa mpenzi wake na pia kuongezea kwamba ana akaunti yake ya benki imejaa hela.
Zari kwa mda sasa, amekuwa akigonga vichwa vya habari pindi tu alipotoa habari za Kingbae, amabaye amedhaniwa kuwa mpenzi wake.
Mama huyo wa watoto watano, hata hivyo, hajawahi onyesha sura ya huyo Kingbae, na wengi husema kuwa ni uongo tu wa kutaka kumfanya mpenzi wake wa zamani apate wivu.
Lakini ni nini kinaweza kuwa kimechangia kwa Zari kuongeza uzito?
Zari anafanya mazoezi ambayo inasaidia kukata mafuta ya mwili inayopatikana katika sehemu ya tumbo na kinamfanya aonekana kama msichana wa umri wa makamo.
Aliongeza pia kwamba mihela kwenye akaunti yake ya benki ndio imechangia kukua vizuri kinachofanya mashabikiwake wapagawe.
Lakini cha kushangazaza ni aliposema kuwa anafanya ngono nzuri ndo kinachompatia maisha ya furaha isiyo na bugdha.
“Watoto wenye afya, chakula kizuri, ngono nzuri, fedha katika benki na amani ya akili. Kila kitu kinanifanya ninenepe”aliandika katika chapisho lake la Snapchat.
Kwa mujibu wa Zari, Kingbae ana pesa kupindukia na amemnunulia nyumba akaihama ile ya Diamond Platinumz akiwa na watoto wake watano ambao wameanza kumpenda ‘Uncle Kingbae’.