Gavana wa Nairobi Mike Mbuvi Sonko atakaa siku mbili zaidi katika ulinzi wa polisi akisubiri uamuzi wa dhamana Jumatano.
Atazuiliwa katika Gereza la Industrial Area Remand Prison kwa siku mbili zaidi.
Court to rule on Governor Mike Mbuvi Sonko & co-accused bail/bond application 11/12/19. All accused persons to be remanded in custody till then. Warrants of arrest issued against suspects not before court today.#GovernorSonko_Prosecution#AntiCorruption_ODPP pic.twitter.com/zsP65pZNqX
— ODPP_KE (@ODPP_KE) December 9, 2019
Sonko Jumatatu alifikishwa mbele ya hakimu mkuu Douglas Ogoti katika Korti ya Sheria ya Milimani ambapo alikana makosa zaidi ya 30 katika kesi ya ufujaji wa pesa takriban Ksh357 milioni.
Nairobi Governor Sonko to spend two more days in police custody pending bail ruling on Wednesday after denying graft charges. https://t.co/1CKwYr1Apu pic.twitter.com/S4oR2jdOjl
— Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) December 9, 2019
Upande wa mashtaka, ukiongozwa na James Kihara, uliimarisha msimamo wake Sonko kupinga ombi lake la dhamana kwa kudai kuwa amewatishia maafisa wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) wakati wa uchunguzi. Na kwamba ana uwezo wa kutoroka nchini.
Prosecution led by James Kihara opposed release of Sonko on bail on grounds that he is a flight risk, is likely to abscond court, intimidate witnesses and interfere with investigations. #SonkoProsecution_ODPP#AntiCorruption_ODPP
— ODPP_KE (@ODPP_KE) December 9, 2019
Waendesha mashtaka wanaoshughulikia kesi yake pia waliiambia korti ya hakimu kwamba Sonko ana kesi ya jinai inayosubiriwa “kwa sababu amekataa kujiwasilisha.”
Tayari, upande wa mashtaka umesema hati ya kukamatwa imetolewa na korti ya Hakimu Mkazi huko Mombasa.
Kwa hivyo, upande wa mashtaka ulisema kwamba ikiwa ataachiliwa kwa dhamana, “Sonko anaweza kuondoka au kuwatishia mashahidi.”
Mwendesha mashtaka alitafuta pia maagizo ya kumzuia Sonko na maafisa wengine wa umma kurudi katika ofisi zao wakisubiri kusikilizwa na uamuzi wa kesi hizo, kuwazuia watuhumiwa kuwasiliana, kuwatisha mashahidi na wachunguzi na, pasi za kusafiria na mahakama.
Prosecution further sought orders-1.Barring Sonko & other public officers from accessing their offices pending hearing & determination of case. 2. Barring accused persons from contacting/intimidating witnesses/investigators. 3. Deposit passports with court
— ODPP_KE (@ODPP_KE) December 9, 2019
Sonko alikamatwa Ijumaa saa nane mchana kwenye kizuizi cha barabara huko Voi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji kutoa hati ya kukamatwa kwake.