Mkuu wa ulinzi Muhoozi David alifanya mkutano mrefu na makamanda wa polisi wa Metropolitan wa Kampala.
Muhoozi alijiunga na makamishna wa polisi wa wilaya, maafisa wa polisi wa upelelezi na polisi wa idara ya uchunguzi wa jinai.
Mkutano huo ulifanywa kwenye makao makuu ya polisi ikiwa nia ni moja tu, kuhakikisha ushirikiano kati ya polisi ili kutoa ulinzi bora kwa wakaazi wa Uganda.
Vigezo ambavyo viliangaziwa kwenye mkutano huo ni pamoja na kutoa huduma bora kwa wananchi, kunaswa kwa majangili, utu kwenye kazi za polisi na msako.
Inspekta wa polisi generali Sabiiti Muzeyi pia alihudhuria akiwa na wakuregenzi wengine wa vituo vya ulinzi nchini Uganda.
Pia kilichozungumzwa pia ni matayarisho ya uchaguzi mkuu wa 2021.
Kwa mujibu wa Info256, kuna viokezo vinaashiria kuwa mkutano huo pia ulidhamiria kuona jinsi ya kuendesha shughuli za uvamizi na mikutano yasiyo na msingi haswa inavyoonekana kwa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change cha Kizza Besigye na mbunge wa Kyandondo Mashariki Bobi Wine.