Wawili wafungwa jela Urusi kwa Hujuma Ukraine

 

Mahakama nchini Urusi imewahukumu wanaume wawili kifungo cha miaka mitatu na miezi sita kila mmoja jela katika kesi ya kwanza ya hujuma tangu Moscow ilipoanzisha operesheni yake ya kijeshi nchini Ukraine, Idara ya Usalama ya Shirikisho la nchi hiyo (FSB) ilisema Jumanne. Wafungwa hao walitambuliwa tu kwa majina yao ya mwisho, Zelenin na Turyansky.

Kulingana na FSB, wanaume hao walizuiliwa Machi 2022 walipokuwa wakipanga kuharibu njia za treni karibu na kijiji cha Tomarovka katika Mkoa wa Belgorod nchini Urusi, ambao unashiriki mpaka na Ukraine.

Wanaume hao walitaka kuangusha treni iliyokuwa ikisafirisha wanajeshi na zana za kijeshi na kusababisha “maafa kwa wanajeshi,” FSB ilisema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *