Waziri wa Afya Mutahi Kagwe Jumapili, Machi 29, alitangaza kwamba visa vinne mpya vya Covid-19 vimethibitishwa nchini Kenya.
Kati ya visa hivyo nne mpya; mmoja ni Mkenya na watatu ni wageni kutoka Amerika, Kamerun na Burkina Faso.
Health CS Mutahi Kagwe confirms 4 more coronavirus cases in Kenya, bringing the total to 42. #COVID19KE pic.twitter.com/Raq50BzckI
— Daily Nation (@dailynation) March 29, 2020
Tangazo hilo linaleta jumla ya visa vyote nchini kuwa 42. Kagwe alihutubia waandishi wa habari katika mkutano na waandishi wa habari nje ya Jumba la Harambee jijini Nairobi.
Kagwe pia alizungumzia maoni ya ubishani yaliyotolewa na mbunge wa Dagoretti Kusini John Kiarie, akimtuhumu mbunge huyo kwa kueneza taarifa potofu juu ya majibu ya serikali juu ya janga hilo.