Basi lililokuwa likisafirisha abiria 46 ambao walikuwa wakielekea kwenye mkutano wa BBI huko Kitui limeanguka na kuingia kwenye mto Waani katika Kaunti ya Makueni Jumamosi, Februari 1.
Ripoti zilionyesha kuwa basi lililoingia kwenye mto uliofurika karibu na soko la Mbiiani mapema asubuhi.
Video iliyopatikana ilionyesha abiria wakijiokoa wenyewe huku wenyeji wakitazama huku wakingoja huduma za dharura.
Kufikia sasa hakuna vifo vilivyoripotiwa.
VIDEO:
Bus Full of BBI supporters Plunges Into Flooded River. @Ma3Route pic.twitter.com/lAuaNkKdVA
— Kenyans.co.ke (@Kenyans) February 1, 2020