Aliyekuwa Mbunge Wa Starehe Charles Rubia Afariki

Mwanasiasa mkongwe aliyewahi kuwa Mbunge wa Starehe Charles Rubia, amefariki.

Image
Charles Rubia

Kulingana na ripoti iliyotolewa na wakili wake, Seneta Irungu Kang’ata, Rubia alifariki akiwa na umri wa miaka 95 katika nyumba yake mtaa wa Karen jijini Nairobi.

Rubia alikuwa meya wa kwanza wa asili ya kiafrika wa jiji la Nairobi.

Baadaye, alichaguliwa kuwa mbunge na kisha kuteuliwa waziri.

Mnamo mwaka wa 1990, pamoja na hayati Kenneth Matiba, walikuwa mstari wa mbele wa kupigania mfumo wa vyama vingi vya kisiasa. alikamatwa na kutiwa mbaroni na aliyekuwa rais, Daniel Moi.

Aliachiliwa kutoka mbaroni baada ya mwaka mmoja na afya yake imekuwa katika hali mbaya tangu wakati huo.

Alikuwa mbunge wa Starehe kati 1969 hadi 1988.

Image result for kenyan parliament

Mnamo Juni, 2019, Rubia aliweka ombo la kulipwa fidia ya KSh 40 bilioni kutoka kwa serikali kufuatia mateso, kufungwa kinyume na sheria.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *