Kiongozi wa ODM, Raila Odinga, Alhamisi, Septemba 19, alivunja ukimya baada ya Rais Uhuru Kenyatta kumpitisha mgombea ubunge wa Jubilee Kibra, McDonald Mariga.
Akiongea kutoka kwa ofisi yake ya Capitol Hill jijini Nairobi, Waziri Mkuu wa zamani alihakikisha kwamba chama chake kilimtanguliza Imran Okoth kama mwakilishi wa chama chao Kibra, na kuongeza kuwa alitetea kampeni za amani kwa ajili ya demokrasia kukomaa.
“Tunapenda kuona kwamba kampeni za Jimbo la Kibra zinafanywa katika mazingira ya amani na ya kirafiki. Hatutaki kuona vurugu za aina yoyote kwenye kampeni hii. Tunataka kuonyesha Wakenya na ulimwengu kwamba demokrasia ya Kenya inakua, “alibainisha.
Waziri Mkuu wa zamani ameongeza kuwa chama chake kitaongoza kwa mfano katika kufanya kampeni za amani.
“Naweza kuwapa hakikisho kuwa ODM itajiendesha kwa njia ya heshima na amani katika kampeni hii,” aliongeza.
Siku ya Jumatano, Septemba 18, rais alimkaribisha mgombea wa uchaguzi mdogo wa chama cha Jubilee, McDonald Mariga kwa ikulu.
Raila Odinga: I assure other parties that ODM is going to conduct itself in a dignified manner during campaigns in Kibra pic.twitter.com/divIRPkLgj
— Citizen TV Kenya (@citizentvkenya) September 19, 2019