Jamaa aliye juu ya gari la polisi akiwa na kaptura avunja mbavu mtandaoni (Video)

Tukio la kustaajabisha lilishuhudiwa katika mji wa Nairobi baada ya mtu aliyevalia kaptura na ‘vest’, alionekana akiwa amepanda juu ya gari la polisi.

Kwenye video ambayo imesambaa mtandaoni, jamaa huyu aliyekuwa juu ya gari anaonekana akiwa amekaa kwa mustarehe gari lilo likipita.

Madirisha ya gari yalikuwa yamepigwa vizuizi, na ikifanya kuwa ngumu kubaini watu waliomo ndani ya gari.

Kwa kushangazwa na tukio hilo, Wakenya wengine walionekana wakisimama kushuhudia tukio hilo la nadra.

Wakenya, kwa hali yao ya kawaida, walipeleka kwenye mtandao wa kijamii kuangazia tukio hilo la kushangaza, wengine wakihoji ikiwa ni kweli maafisa wa polisi walikuwa ndani ya gari.

“Picha ya nadra ya mlipa kodi akisherehekea pesa zake,” mmoja alisema.

 

View this post on Instagram

 

Vile kesho tunaingia Luo Festival…

A post shared by JALANG’O (@jalangoo) on

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *