Waziri Ummy Mwalimu aonya kuhusu utapeli

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu  amewataka wananchi kua makini na taarifa  za uvumi zinazoendelea kuhusu mikopo inayotolewa na WEKEZA SACCOSS ikimuhusisha yeye.

Waziri Ummy aliandika katika ukurasa wake wa mitandao ya kijamii wa Instagram na Twitter na kufafanua kwamba hausiki na Mikopo yoyote inayodaiwa kutolewa na WEKEZA SACCO’S au Taasisi nyingine yoyote.

Wazir Ummy ameliomba Jeshi la Polisi kuwachukulia hatua kali wote wanaofanya udanganyifu huo.

Posti ya mtandao wa kijamii wa twitter ya Waziri Ummy Mwalimu ikionyesha taarifa inayosambaa ikidai anahusika na mikopo hii hapa:

Aidha, tabia hizi za utapeli si mara ya kwanza kwani jina la Mke wa Rais John Magufuli, Mama Janeth Magufuli lilishawahi kutumika katika akaunti ya mtandao wa kijamii wa Facebook kudanganya watu waombe mikopo.

Kufuatia  hali hiyo Msemaji wa mkuu wa serikali alitahadharisha wananchi kuipuuzia akaunti hiyo May 30 mwaka huu kupitia akaunti ya tweeter isome hapa chini

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *