Msanii wa mziki wa kufokafoka Eko Dydda amepuuzilia mbali madai ya mashtaka kutoka kimapenzi nje ya ndoa baada ya mke wake kumshutuma hadharani.
Rafiki wa karibu wa familia ya Eko Dyda anasemakana kukukuwa na uhusiano na msanii huyu wa injili kilichopelekea kusambaratika kwa ndoa yao ya miaka tisa.
“Kuvunja ndoa ya mtu sio vyema, nimekualika wewe kama rafiki, leo unasema ambia Eko Dydda asinilete nyumbani kwa sababu upendo wenu haita kua, “Cynthia aliandika.
Kwa mujibu wa Cynthia, walikuwa na masuala ya ndoa na alimtafuta rafiki wa karibu, lakini cha kushangaza alipata kujua kuwa rafiki alikuwa ana uhusiano na Eko Dydda.
“Baada ya miaka tisa, nimeamua kutoka kwa ndoa na naishi mahali tofauti. Pia, nataka Eko ajue kwamba ako huru kuendelea na mwanamke ‘DOPE’ katika maisha yake. Pia nataka ulimwengu kujua kwamba si kila rafiki anayepaswa kuaminiwa, “aliongeza.
Kisha baadaye itajitokeza kuwa mwanamke aliye katika suala hilo ni Rapa LC, ambaye Eko Dydda anasema amekuwa rafiki wa karibu kwa familia kwa muda mrefu lakini anakataa kushirikiana kimapenzi.
Eko Dydda alikuwa anazungumza na Monday Blues ambapo hakutaka kuongezea mengi.