Tumeshuhudia mastar wengi duniani baada ya kuachana na wapenzi wao ,wengi wao hupenda kujitenga kwa muda na masuala ya publicity ,wengine hufanya sherehe na wengine hata kusafiri na kwenda vacation.
Sasa sikia hii nyota wa filamu nchini Tanzania ,Shamsa Ford ameonekana Dubai akila bata la nguvu hii ni baada ya kuachana na mumewe Chid Mapenzi .
Mwanzoni mwa mwezi huu zilikuwepo tetesi juu ya wawili hao kuachana na kisha kuthibitishwa na Shamsa mwenyewe kupitia akaunti yake ya Instagram.
Watu wengi wameonekana kujuiuliza je bata analokula Shamsa huko Dubai ni njia ya kuondoa msongo wa mawazo au kapata mpenzi mwingine.
We unaonaje? Shuka hapo chini!