Leo ndio maadhimisho ya mwisho ya Kitaifa ya Rais Jomo Kenyatta- Uhuru

President Uhuru Kenyatta, First Lady Margaret Kenyatta at the mausoleum of founding President Mzee Jomo Kenyatta on August 22, 2019.

Rais Uhuru Kenyatta Alhamisi alitangaza kuwa kumbukumbu ya 41 ya baba mwanzilishi wa nchi Mzee Jomo Kenyatta itakuwa ya mwisho.

Uhuru alisema makubaliano hayo yaliafikiwa baada ya mashauriano na familia nzima ya Kenyatta. Uhuru ameongeza kuwa kama familia watakuwa wakifanya sherehe ya  kibinafsi kama wanafamilia kusonga mbele.

“Kama Rais, nimeshauriana na familia ya Mzee Kenyatta. Tumekubaliana kwa pamoja kwamba hii itakuwa sherehe ya mwisho ya kumbukumbu ya Mzee kwa njia hii,” alisema.

President Uhuru Kenyatta and First Lady Margaret Kenyatta lay a wreath of flowers at the mausoleum of founding President Mzee Jomo Kenyatta on August 22, 2019.

Alizungumza wakati katika Kanisa la Holy Family Basilica alipokuwa akiongoza taifa katika kumkumbuka za baba mwanzilishi wa taifa. Rais ameongeza kuwa nchi imesonga mbele katika miaka 41 na na kushuhudia mabadiliko na maboresho makubwa.

Pia aliwapa shukrani  Marais wote wawili waliomtangulia kwa kuzingatia kama ibada maadhimisho ya Mzee Kenyatta bila kukosa.

Mzee Jomo Kenyatta alikufa mnamo Agosti 22, 1978.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *