Bwana mkunaji ama kwa jina la kisanii Willy Paul ameelezea jinsi alivyokerwa na rafiki wake wa karibu, msanii wa Jamaica, Alaine.
Willy Paul ameamua kufungua roho na kuonyesha vile amekuwa akipuuzwa na msanii huyo wa kike.
Msanii wa injili anasema kuwa Alaine amekuwa akimpuuza kwa muda sasa na hii ilidhihirika siku ambayo alifika nchini bila ata kumsemezea wala kumtafuta.
Itakumbukwa kuwa Willy Paul na Alaine waliunda msingi wa urafiki wao miaka chache iliyopita walipofanya mziki wa pamoja kwenye ‘I do’ ambayo ilikuwa mziki mkubwa Afrika ya Mashariki haswa kwa maharusi.
Wafuasi wao wamekuwa wakiamini kuwa urafiki wao ni mkubwa haswa walipoonekana kwenye picha za hivi karibuni walipokutana na kuonekana wamejawa na furaha.
Lakini Pozze amekiri kuwa mambo hayako sawa vile maanake Alaine amemtoa kwenye simu yake na hakuna mawasiliano kati yao.
“Siku hizi haushiki simu yangu, nakutumia ujumbe lakini haunipi jibu lolote. Nimekukosea kwa jambo lolote lile? Hapana, sidhani ni hivyo, majuma yaliyopita ulifika Kenya na hukunitafuta wala kunisemezea,” Willy Paul alilaani.
Je kunaweza kuwa kumetokea msukosuko mahali?
Willy Paul anaamini Alaine alisikia na kujionea ukaribu wa Nandy na Pozze akafikiria wawili hao wanachumbiana kitu ambacho msanii wa injili amekana.
Aliweka wazi kuwa wawili hao ni marafiki wa karibu tu na hakuna kinachoendelea kati yao mbali na biashara.
Nandy amekuwa akionekana na Willy Paul wakifanya matamasha ya kufana na michezo yao ya ‘Sellina’ kwenye jukwaa si wa kiinjili ata kidogo bali ni ya kidunia kitu kilichofanya wengi kushuku uhusiano wao.
Willy Paul ameomba wafuasi wake kumsaidia kupitisha ujumbe kwa Alaine kwamba yeye ameathirika sana na kimya chake.
Kwa hiyo ni sawa kusema mambo ya mkunaji ni hadithi tu?
Haya ni baadhi ya maoni ya wauasi wake;