Mbunge wa Mashariki wa Kyandondo upande wa Uganda Robert Kyagulanyi almaarufu Bobi Wine alisafir kwa mji wa Amsterdam mahali alikuwa na tamasha yakuburudisha mashabiki wake na pia kukuza nchi yake ughaibuni.
Bobi Wine aliwashukuru wote wenye walifika kwenye ukumbi huo kwenye mji wa Amsterdam.
“Asante marafiki wote waliotoka sehemu zote za Uropa kujiunga nami kwenye ukumbi huu hapa Amsterdam leo usiku. Imekuwa vyema sana kuonana na natumai tamasha hii itakuwa wa kufana zaidi na bendi yangu.”
Akiendelea na mambo ya mziki, hakukosa kugusia nchi yake ya Uganda na pia kuwapongeza raia wa Uganda ambao wanaishi ughaibuni na bado wana uzaleno mkuu.
“Ujumbe wangu ni hii, ukiwa upo Uganda au ng’ambo, lazima tupiganie uhuru wa nch yetu,” aliongezea.
Aliongeza kuwa kila kizazi kina wajibu wa kutekeleza ile kuwe na kizazi kizuri kichacho.