Mke wa Mwimbaji tajika wa injili Eko Dydda ameipa kisogo ndoa yao.
Kupitia mtandao wa kijamii, Cynthia Ayugi alimshtaki bwana wake kwa kulala na mwendani wake.
Kuvunja ndoa ya mtu sio sawia na maandiko, nimekualika wewe kama rafiki, leo unasema ambia Eko Dydda asinilete nyumbani kwa sababu upendo wenu haitakua
Cynthia aliyeonekana ana hasira tena alisema kwamba hakutaka kuweka siri ya uaminifu wa Eko Dydda kwa ajili ya umaarufu.
“Sio vita, @ekodydda hamna haja kujificha tena, ‘DOPE’ wako ana huru kukupenda, wakati mwingine ni heri kuondoka.”
Na leo ndio siku, sitakuficha kwa umaarufu, pesa, nitasimama na ukweli na kamwe sitadanganya watu
Kwa mujibu wa Cynthia, walikuwa na masuala ya ndoa na wakatafuta marafiki wawasaidie kutatua lakini alipigwa na butwaaa alipoelewa kwamba rafiki wake alikuwa anatoka kimapenzi na Eko Dydda.
“Sikujua kwamba walikuwa tayari katika uhusiano. Nilijifunza baadaye baada ya Eko Dydda kulala nje na nilipowapigia wote wawili hawakupokea simu yangu, “aliiambia The Word Is.
Hii ilitokea baada ya Eko Dydda kukataa madai ya kuvunjika kwa ndoa yao miezi miwili iliyopita.